• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Idara ya Fedha na Biashara kuboresha ukusanyaji mapato Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: April 24th, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imewataka maafisa watendaji kata kujiamini na kuhakikisha lengo la ukusanyaji wa mapato ya halmashauri linafikiwa ili serikali iweze kutoa huduma bora kwa wananchi wake.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mweka Hazina wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA Rahabu Philip (pichani) alipokuwa akiongea na maafisa watendaji wa kata za jiji hilo katika kikao cha kawaida cha kukumbushana wajibu wa maafisa watendaji wa kata katika kukusanya mapato ya halmashauri.

CPA Philip alisema kuwa maafisa watendaji wa kata wana wajibu wa kusimamia ukusanyaji wa mapato ya halmashauri katika kata zao. “Maafisa watendaji wa kata ndiyo vidole vya Mkurugenzi wa Jiji, na bahati nzuri vyanzo vyote vya mapato vipo katika kata zenu. Mkurugenzi hana kata ya kukusanya mapato. Ushuru wa huduma unapatikana kwenye kata, ushuru wa hoteli unapatikana kwenye kata, ushuru wa madini ujenzi unapatikana katika kata. Hivyo, mnatakiwa kujiamini katika kutekeleza majukumu yenu” alisema CPA Philip.

Akiongelea uvujaji wa mapato ya halmashauri, alisema kuwa wote wakitimiza wajibu hakuna mapato yatakayovuja. “Hata tunapoongelea uvujaji na upotevu wa mapato ya halmashauri, mtu wa kwanza kufahamu uvujaji huo ni mtendaji wa kata, hivyo wajibu wenu katika kuhakikisha serikali inakusanya mapato yake ni mkubwa sana” alisisitiza CPA Philip.

Kwa upande wake, Afisa Biashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Donatila Vedasto aliwakumbusha maafisa watendaji hao kusimamia ukusanyaji wa leseni za biashara. “Ukusanyaji wa leseni za biashara ni jukumu letu sote. Maafisa biashara hatuwezi kufika katika maeneo yote ya halmashauri, ila maafisa watendaji wa kata kwa kushirikiana na maafisa watendaji wa mitaa tunaweza kuyafikia maeneo yote ya biashara” alisema Vedasto.

Aidha, aliwataka kuwatambua wafanyabiashara wote waliopo na wanaoanzisha biashara mpya ili waweze kukata leseni na serikali kupata mapato yake. Alisema kuwa halmashauri imeanzisha utaratibu wa kupata taarifa za kila robo kufahamu idadi ya leseni zilizokatwa, idadi ya leseni zilizoisha muda wake na idadi ya leseni zilizohuishwa kutoka katika kata.

 Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina kata 41 na jumla ya mitaa 222.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.